Jumanne , 16th Aug , 2022

Mwanaume mmoja nchini Nigeria mwenye umri wa miaka 42 anapambania kuokoa maisha yake baada ya kuzikata sehemu zake za siri na kisu ndotoni, baada ya kuota anachinja mbuzi kwa ajili ya kumsaidia mke wake kuandaa chakula cha jioni.

Kisu

Tukio hilo limetokea Agosti 12, 2022, na kusema kwamba baadaye alikuja kushtuka na kugundua kwamba alikuwa akizikata sehemu zake za siri badala ya mbuzi kama alivyokuwa anaota.

Imeelezwa kwamba mke wa mwanaume huyo hakuwepo nyumbani na ndipo alipopigiwa simu na majirani zake kumuarifu kwamba mume wake amejeruhiwa na ndipo alipowahi kurudi nyumbani na kumkuta amezishikilia sehemu zake za siri na kisha kumpeleka hospitali.