Jumatatu , 27th Sep , 2021

Ni wazi kuwa Smartphone zimekuwa ni sehemu ya maisha ya watu wengi kila siku, lakini ni vizuri ukafahamu kuwa washauri wa masuala ya Teknolojia wanasema ku-restart (kuwasha tena) simu yako angalau mara moja kwa wiki kunarahisisha utendaji kazi wa kifaa hicho.

Picha ya Simu

Bob Motamedi ambaye ni mshauri wa teknolojia anasema kufanya hivyo husaidia simu kudumu na chaji lakini pia kufanya kazi haraka na vizuri zaidi ukilinganisha na simu ambayo hauja-restart.