18 kuwakilisha Tanzania Afrika kanda ya 3
Chama cha kuogelea Tanzania TSA kimesema kuwa kinataraji kupeleka waogeleaji 18 katika michuano ya ubingwa wa Afrika kanda ya tatu na nne itakayofanyika jijini Kampala Uganda kuanzia April 24 mwaka huu.
Katibu mkuu wa TSA Noel Kihunsi amesema kuwa wachezaji wote hao tayari wako katika maandalizi mazito katika vilabu vyao hapa nchini na wale walioko nje ya nchi nao wanaendelea na mazoezi kama kawaida.