Mbunge akanusha kuhusika na uwindaji haramu
Mbunge wa Tunduru mkoani Ruvuma nchini Tanzania, Mtutura Abdallah Mtutura, amesema pembe za ndovu zinazokamatwa jimboni kwake ni za tembo wanaouwawa katika mbuga ya Niasa nchini Msumbiji na si jimboni kwake kama ambavyo wengi wamekuwa wakidhania.