Watanzania 15 wanasubiri kunyongwa nchini China
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Tanzania imesema hadi kufikia Februari mwaka huu watanzania 177 wamefungwa katika magereza nchini China, huku miongoni mwao 15 wakiwa wamehukumiwa kunyongwa kutokana na makosa ya dawa za kulevya.