Mwisho kuchukua fomu za uchaguzi TSA Septemba 30.

Fomu kwa ajili ya nafasi za kugombea uongozi wa chama cha kuogelea Tanzania TSA zimeanza kutolewa kwenye Baraza la michezo Tanzania BMT, na Baraza la michezo Zanzibar BMZ.

Afisa Habari wa BMT Najaha Bakari amesema,fomu hizo zimeanza kutolewa tangu Septemba 10 na mwisho wa kuchukua fomu hizo ni Septemba 30 mwaka huu,ambapo ametoa wito kwa wadau wa mchezo wa kuogelea kujitokeza kuchukua fomu hizo ili kuongoza chama hicho na kuleta maendeleo katika mchezo huo.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS