Mwenyekiti wa Mviwata Veronika Sophu akizungumza na waandishi wa habari wanaoandika habari za wakulima (kulia) ni Mkurugenzi wa Mviwata Stephen Ruvuga.
Wakulima wadogo nchini wameiomba serikali kuwaandaa katika kuingia kwenye ushindani wa soko la kimataifa ili kuwawezesha kushindana na nchi nyingine katika ubora wa bidhaa wanazozalisha .