NEC Yavitaka vyama vya siasa kukubali matokeo
TUME ya Taifa ya Uchaguzi ( NEC) imesema hadi sasa viti maalumu vya Udiwani ambavyo madiwani wake wameteuliwa na tume hiyo ni viti 1393, kutoka katika Vyama vya CCM, CHADEMA, NCCR- MAGEUZI pamoja na CUF.
Hayo yamesemwa jijijini Dar es Salaam na mkurugenzi wa uchaguzi kutoka NEC Bw. Kailima Ramadhani wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu uteuzi wa madiwani wanawake wa viti maalumu.