Tanzania yapanda nafasi 4 kwa uwekezaji duniani
Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika eneo la uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji ambapo kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa jijini Dar es Salaam leo, Tanzania imepanda kwa nafasi nne ikishika nafasi ya 116 kati ya nchi 138 zilizofanyiwa utafiti.