BASATA yafungukia kuhusu malipo ya wasanii
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limefunguka na kutolea ufafanuzi kanuni zake mpya walizozifanya hivi karibuni kuwa sio kweli kwamba msanii anatakiwa kulipa milioni 5 akifanya tangazo bali kampuni husika ndio inapaswa
kufanya hivyo kwa kuwa wanaingiza kipato kikubwa kutumia tangazo hilo.