JKT Tanzania wakoshwa na uteuzi wa Rais Magufuli
Klabu ya soka ya JKT Tanzania inayoshiriki ligi kuu soka Tanzania Bara, imeeleza kufurahishwa na uteuzi wa Rais Magufuli ambaye jana Desemba 7, 2018 alimteua Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).