Baada ya hukumu kufutwa Sugu aeleza kinachofuata
Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, amesema kuwa atakaa na mawakili wake ili kujua nini cha kufanya kwa lengo la kuhakikisha hakuna mwananchi mwingine anafungwa kiholela kama alivyokuwa amefungwa yeye.

