Mhubiri amuua mkewe wakati wa ibada
Mhubiri Elisha Misiko wa kanisa la Ground for Jesus, lililoko mjini Mombasa nchini Kenya, amemuua mke wake kwa kumchoma na kisu na kisha yeye kujikata koo lake na kufariki papo hapo, wakati wa ibada ya Jumapili ikiendelea kanisani hapo.

