
Rais Samia Suluhu Hassan
Kupitia ukurasa wake wa X Rais Samia ameambatanisha barua hiyo yenye ujumbe wa Papa Francis ambao alikabidhiwa Balozi wa Vatican hapa nchini.
"Kwa unyenyekevu na shukrani, nimepokea ujumbe wa hayati Papa Francisko kwangu, kwa nchi yetu na kwa Watanzania wote, aliouandika siku chache kabla Mwenyezi Mungu hajamwita kwake, na kumkabidhi Balozi wa Vatican hapa nchini, Askofu Mkuu Angelo Accattino. Tuendelee kumwombea kwa Mwenyezi Mungu alale mahali pema," ameandika Rais Samia