Thursday , 22nd Aug , 2024

Uongozi wa Simba SC umethibitisha kumuuza mshambuliaji wa Fredy Michael Koublan kutokana na kushindwa kumshawishi mkufunzi mkuu wa Simba SC Fadlu Davids kuelekea msimu huu wa mashindano 2024-25.

Akizungumza na EATV Meneja Habari na Mawasiliano Simba SC  Ahmedy Ally amekiri kuwa mchezaji huyo kuuzwa nchini Algeria  huku upande mwingine ameweka wazi kuhusu maendeleo ya golikipa Ayoub Lakred aliyepata majeraha nchini Misri.

''Fredy Michael alikuwa na mkabata na Simba SC hivyo tumemuuza katika klabu hiyo ya nchini Algeria na ndani ya wiki hii tunakwenda kuwatangazia wanasimba ni timu gani ambayo amekwenda''amesema Ahmedy Ally.

Timu ya Simba SC inayoongoza kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara msimu huu,itarajiwa kushuka dimbani Agosti 25 , 2024 dhidi ya  Fountain Gate FC katika mchezo utaopigwa majira ya saa 10 jion katika uwanja wa KMC Complex, Mwege , jijini Dar es salaam