Shadrack Chaula
Ikumbukwe kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga,Julai 2 mwaka huu ilieleza kuwa mnamo Juni 30, 2024, mtuhumiwa huyo ambaye ni msanii wa sanaa ya uchoraji alijirekodi video fupi akitamka maneno makali ya kumkashifu Rais Samia huku akichoma picha inayomuonesha Rais na kuisambaza mitandaoni.