Tuesday , 5th Mar , 2024

Watumiaji wa mitandao ya kijamii ya Instagram na Facebook wamepigwa na butwaa baada ya mitandao hiyo kupotea ghafla jioni ya leo Machi 5, 2024.

Facebook na Instagram

Baadhi ya watumiaji wa Facebook wameripoti kuwa account zao zime- log out zenyewe na hata wakijaribu kuingiza neno la siri bado hakuna mafanikio huku upande wa Instagram watumiaji wakikutana na maneno yasemayo 'no internet connection au failure to load'

Kupitia mtandao wa ''X'' msemaji wa META Bwana Andy Stone alikiri kuwapo kwa changamoto kwenye mitandao ya META na kusema kuwa wanashughulika na changamoto hiyo.