Thursday , 25th Jan , 2024

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme ametangaza rasmi operesheni maalum ya kuondoa madada poa wanaojiuza mkoani humo lengo likiwa ni la kulinda maadili ya vijana.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme

RC Mndeme ametangaza hilo wakati akizungumza kwenye kikao na wazee, machifu na viongozi wa dini kutokana na wazee mkoani humo kulalamikia biashara ya ukahaba kuzidi na kusababisha mmomonyoko wa maadili kwa vijana.

Kwa mujibu wa RC Mndeme, msako wa madada poa hao umeanza rasmi jana hivyo amewataka wahusika kuacha biashara hiyo mara moja.