
Wakipigana mabusu
Kitendo cha wawili hao kubusiana wodini kimefanyika jana Julai 9, 2023, ambapo video hiyo ilirekodiwa na mmoja wa wagonjwa aliyekuwa katika kitanda cha jirani.
Aidha Taasisi hiyo imesema kwamba mpenzi wa mgonjwa huyo si mtumishi wa MOl.
"Menejimenti ya MOI inalaani kitendo hicho cha uvunjifu wa maadili kilichofanywa na mgonjwa huyo pamoja na mpenzi wake, vilevile Menejimenti inalaani na kukemea kitendo cha kurekodi video wodini na kutuma kwenye mitandao ya kijamii kilichofanywa na mgonjwa jirani, matukio haya yote ni kinyume na mwongozo wa Wizara ya Afya unaozuia kufanya matendo ya uvunjifu wa maadili kwa mgonjwa na kurekodi video wodini," imeeleza taarifa iliyotolewa na Mvungi ambaye ni Meneja Uhusiano MOI
Pamoja na hayo yote menejimenti inaendelea kuchunguza zaidi tukio hilo ili kujiridhisha kuwa hapakuwa na uzembe katika kusimamia usalama wa wagonjwa wakati ndugu wanawatembelea wagonjwa wodini.