Monday , 3rd Jul , 2023

Mahakama Kuu kanda ya Mbeya imesogeza mbele hadi tarehe 20 Julai 2023 kesi namba 5/2023 ya Wadau  wa katiba ya kuhoji uhalali wa mkataba uliosainiwa na Serikali ya Tanzania

na kupitishwa na Bunge kwa kutengeneza sheria zitakazotumika kuongoza mikataba ya Ubinafsishaji wa bandari  kwa kampuni ya DP World ya Dubai hadi Julai 20 mwaka huu

Kesi hiyo ambayo imepangwa kusikiliwa na majaji wa tatu ilikuwa inasikiliwa na jaji Dustani Nduguru ambapo Wajibu Maombi (Wakili Serikali) waliomba mahakama isogeze mbele ili kupata fursa ya kukusanya vielezo vya waleta maombi baada ya mvutano wa mda mrefu Mahakama amewaaigiza wajibu na waleta maombi kuwasilisha nyaraka Julai 14 ili kesi ianze kusikilizwa mfululizo kuanzia Julai 20

Kesi hiyo imefunguliwa Mahakama kuu kanda ya Mbeya na Emmanuel Kalikenya Chengula, Alphonce Lusako, Raphael Japhet Ngonde na Frank John Nyalusi wakimshtaki mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri wa Uchukuzi,katibu wa Wizara ya Uchukuzi na katibu wa Bunge 

Kesi hiyo inasimamiwa na mawikili wa kujitegemea Bonface Mwabukusi, Philip Mwakilima, Livino Haule na Caroline Luhungu.

Mawakili wa Serikali ni Hangi chanya Wakili wa serikali Ayoub Sanga  wakili wa Serikali (SA)
Kesi hiyo inasikiliwa na majaji watatu wa Mahakama kuu

Majaji wengine walipongiwa kusikiliza kesi ya kikatiba ni Abdi S Kagomba (mahakama Kuu Dodoma

Akizungumza nje ya Mahakama mmoja wawalamikaje Alphonce Lusako asema amesema sababu ya kugungua kesi hiyo ni kutaka kupata tafsiri kisheria na kwamba hawapinga suala la uwekezaji lakini wanapinga baadhi ya vipengele vilivyopo kwenye mkataba huo.