Monday , 3rd Jul , 2023

Wadau wa Katiba Emmanuel Chengula, Alphonce Lusako, Raphael Ngonde na Frank Nyalusi wamefungua kesi katika Mahakama kuu kanda ya Mbeya wakiwashtaki mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri wa Uchukuzi, Katibu wa Wizara ya Uchukuzi na katibu wa Bunge

Wadau hao wanahoji uhalali wa mkataba uliosainiwa na Serikali ya Tanzania na kupitishwa na Bunge kuhusu uwekezaji bandarini

Wadau hao wa katiba wanahoji uhalali wa mkataba uliosainiwa na Serikali Jamuhuri ya Tanzania na kupitishwa na Bunge kwa kutengenzea sheria zitakazo tumika kuongoza mikataba ya uwekezaji bandarini  kwa kampuni ya DP World ya Dubai

Kesi hiyo inasimamiwa na mawikili wa kujitegemea Bonface Mwabukusi, Philip Mwakilima, Livino Haule na Caroline Luhungu