
Esther Mkombozi , aliyepata madhara baada ya kuchoma sindano duka la dawa
Hatua hiyo imekuja kufuatia video moja kusambaa mitandaoni ikimuonesha Esther Mkombozi mkazi wa Arusha aliyeeleza kuwa alichomwa sindano katika duka la dawa na kumsababishia madhara katika mkono wake.
"Tunampa pole Esther kutokana na madhara aliyopata, tuwaombe wananchi kuendelea kuwa watulivu ambapo suala hill linafanyiwa kazi," imeeleza taarifa ya Wizara ya Afya
Kutokana na hilo, Wizara imeelekeza Baraza la Famasi (PC) na Bodi ya Hospitali Binafsi (PHAB) kufuatilia suala hilo mara moja na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wote watakaobainika kukiuka sheria, kanuni, miongozo na Taratibu za Usimamizi na Udhibiti wa utoaji wa huduma za Afya nchini.