
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Kauli hiyo ameitoa hii leo Aprili 14, 2023, bungeni jijini Dodoma wakati akitoa tamko kufuatia hoja iliyojadiliwa bungeni humo kuhusu vitendo vya mmomonyoko wa maadili na vitendo vinavyokwenda kinyume na mila, tamaduni na desturi za Mtanzania.
"Sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 ya sheria ya Tanzania inatamka bayana kwamba vitendo vya mapenzi ya jinsia moja au kinyume na maumbile iwe kwa faragha au kwa makubaliano ni kosa la jinai," amesema Waziri Mkuu
Waziri Mkuu amesema kwamba uwepo wa matukio na vitendo hivyo umekuwa ukihatarisha uimara na ustawi wa familia na Taifa kwa ujumla.
Tazama video hapa chini.