
Picha inayoonesha baadhi ya vifaa vya kufanyiwa upasuaji
Dkt. Humba ameyasema hayo leo Julai 21, 2022, Jijini Dodoma mara baada ya kukutana na wataalamu wa upasuaji wa viungo vya binadamu ikiwemo nyonga, mifupa, mishipa ya fahamu na ubongo kutoka Hospitali ya kibingwa ya Apollo nchini India, kwa lengo la kubadilishana ujuzi wa kibingwa katika sekta ya afya kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Kwa upande wake Daktari bingwa wa mfumo wa fahamu ,nyonga na ubongo kutoka Hospitali ya Apollo India Dkt.Ruthiramurthy Irish, amesema wamekuja Tanzania kubadilishana utaalamu wa kibingwa bobezi wa mifupa kwa kuwa ni moja ya nchi inayoonekana kufanya vizuri pindi inaposhirikishwa katika sekta ya afya.