
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho
Amesema kuwa kujiuzulu kwa Job Ndugai haimaanishi kwamba yeye sio kiongozi mzuri lakini hakuchagua maneno ya kusema na kwa wakati gani na akiwa nje atajitafakari na kujifunza.
Aidha, Mwisho amesema kuwa CCM haiwezi kugawanyika kwa sababu hakuna aliye mkubwa kuliko chama hicho, na kwamba bado kipo imara.