Tuesday , 10th Aug , 2021

Msanii wa Injili Bongo Goodluck Gozbert amesema ni sawa kwa muziki huo kupigwa kwenye kumbi za starehe kwa sababu ma-dj wengi ni wakristo na walokole hivyo ziendelee kupigwa tu.

Msanii Goodluck Gozbert

Akifunguka kupitia show ya eNewz ya East Africa TV Goodluck Gozbert anasema muziki huo kuchezwa Club inaongeza ujumbe ambao mtu hachagui kuusikia.

"Ma-dj ni wakristo walokole huwezi  kuwazuia kupiga muziki wa nyumbani kwao nahisi ni sawa acha zidundwe tu, haipunguzi chochote bali inaongeza kitu kwa sababu ni ujumbe ambao mtu hachagui kuusikia kama ambavyo mtu hachagui pa kufanya sala" ameeleza

Zaidi tazama hapo chini kwenye video.