
Picha Msanii Dayna Nyange
Dayna ameweka wazi kuwa baada ya kuachia wimbo wake “Elo” aliomshirikisha Davido kutoka Nigeria kutoka kwenye EP hiyo amabyo ni ya kwanza kutoka kwake, sasa ni wakati wa kuipeleka sokoni.
“I am so thrilled and excited kukujulisha kwamba my first E.P. Titled “Elo” itoka kesho 17 June, Can’t wait for you to listen and vibe to the songs in the EP and get the chance to taste what I’ve been cooking for some time now”. – ameandika Dayna.
EP hiyo ina jumla ya nyimbo 4 ambazo ni Teketea, Shona, Maujuzi na Elo ambayo ilitoka Mei 28, 2021 huku Kesh Ofuobi, Mr T, Mocco Genius na Napji ndio watayarishaji waliohusika katika kuipika.