
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako
Prof. Ndalichako ametoa ombi hilo katika Kongamano la Kimataifa kuadhimisha miaka 50 ya elimu ya watu wazima Tanzania, ambapo amesema elimu ya watu wazima ni muhimu kwa nchi yetu.
"Kila Halmashauri tunakuwa na afisa elimu ya watu wazima, kuna baadhi ya maeneo elimu ya watu wazima imelala, kila mmoja ajitathimini katika halmashauri yake wanafanya nini na wanamipango gani kuhusu elimu ya watu wazima, naomba TAMISEMI katika mambo yote ya kipaumbele hebu twende na elimu ya watu wazima," amesma Prof. Ndalichako.
Aidha, Prof. Ndalichako amesema kuwa wataandika pendekezo kwa Waziri Mkuu kuhusu maafisa elimu ya watu wazima ambao hawafanyikazi.
"Tunapopokea taarifa, tupate pia na taarifa ya elimu ya watu wazima, vinginevyo Mhe. Waziri Mkuu tutaandika pendekezo maafisa elimu ya watu wazima ambao hawafanyi kazi tuwagawe bure katika maeneo mengine yanayohitaji watu wachapakazi," amesema Waziri Ndalichako.