
Mbunge wa Bunda Vijijini Peter Mwita Getere
Kauli hiyo ameitoa leo Mei 28, 2021, Bungeni Jijini Dodoma wakati akiuliza swali lake kwa Wizara ya Maliasilia alipotaka kujua idadi ya Tembo wanaopaswa kuishi kwenye mapori ya Tanzania.
"Haya mambo ya wanyamapori mimi naona sasa tunakokwenda tutabakiza nchi ya wanyamapori, najiuliza hivi ni Tembo wangapi wanatosha kuishi katika mapori ya Tanzania ambao watalii watakuja kuona kama Tembo hawa hawana uzazi wa mpango," ameuliza Mbunge Getere.