Rais Magufuli kwenye picha kubwa na picha ndogo ni kikosi cha Taifa Stars
Magufuli ametoa kauli hiyo leo Desemba 9, 2020 wakati akiapisha Mawaziri katika hafla iliyofanyika jijini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa wakati umefika kuachana na mazoea ya vilabu vya Simba na Yanga.
''Wizara ya Michezo tumekupeleka Bashungwa ili tukacheze kweli, tumekupeleka huko tunataka tukashinde kweli, tukienda kucheza tukafungwa sijui magoli 10 mtaondoka wote Waziri na Naibu Waziri'' - Dkt. Magufuli
Magufuli ameongeza kuwa, ''Tunataka tuwe na timu ya taifa inayoshinda na mambo ya kwenda na Simba na Yanga tu tumechoka inawezakana umefika wakati tuwe na timu ya taifa ambayo haina uhusiano na Simba na Yanga''.

