
Faru Fausta
Naibu Waziri Kanyasu amesema moja ya sababu ya kifo cha Fausta ni uzee ambapo kwa sasa ana miaka zaidi 56, huku akiwa na watoto na wajukuu wengi.
Kanyasu amesema kuwa " Ni kweli Faru Fausta amefariki Dunia tena akiwa na miaka 56 na amefariki sababu ya kuishi muda mrefu"
"Kama Wizara tunashirikiana na wanasayansi ili kuangalia namna ya kumuhifadhi huyu Faru kwa kuwa ameingizia Taifa pesa nyingi sana." amesema Kanyasu
#HABARI Naibu Waziri wa Utalii, Constantine Kanyasu, amesema baada ya Faru Fausta kufariki wanashirikiana na baadhi ya wanasayansi ili kuangalia namna ya kuhifadhi mwili wa mnyama huyo, ili uendelee kuwa kivutio kwa Watalii. pic.twitter.com/WGcjyVozfv
— East Africa TV (@eastafricatv) December 28, 2019