Wednesday , 1st Jun , 2016

Baada ya timu ya Kagera Sugar kunusurika kushuka daraja, uongozi wa timu hiyo iliyopo mkoani Kagera unatarajia kumtangaza Mecky Mexime kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo.

Aliyekuwa Kocha wa Mtibwa Sugar Mecky Mexime

Mexime anatarajia kuchukua mikoba ya Adolph Rishard ambaye uongozi wa timu hiyo haujaridhishwa na kiwango chake cha kazi.

Kwa upande wa Mtibwa Sugar pia inatarajia kumrejesha aliyekuwa kocha wake Mkuu Salum Mayanga ambaye msimu uliomalizika alikuwa akiifundisha Tanzania Prisons ya jijini Mbeya ambayo ilimaliza ligi ikiwa kwenye nafasi ya nne kwa kubeba pointi 51.