Kwa upande wa pili wa michuano hiyo, Mabingwa watetezi wa Kombe hilo, Timu ya Azam Fc itaikaribisha Ruvu Shooting Uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam.
Katika muendelezo wa Ligi hiyo, Yanga itakutana na Mbeya City ya jijini Mbeya mechi itakayopigwa mwishoni mwa juma hili.
Msemaji wa Mbeya City, Dismas Ten amesema, baada ya kulazimishwa sare katika mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union jijini Tanga, sasa hasira zao wamezielekeza kwa Yanga.
Ten amesema, Licha ya Yanga kupata ushindi dhidi ya BDF, wanaamini watawafunga na wasitarajie kuondoka na Pointi hata moja.


