
Twiga Stars
Afisa habari wa Shirikisho la Soka nchini TFF, Alfred Lucas amesema, hapo awali Cameroon waliomba mchezo mmoja lakini wameomba kuchezwa michezo miwili ambapo wamekubaliana nao kwani wanaamini michezo hiyo itakuwa ni kipimo kizuri kwa Twiga Stars kwa ajili ya michuano mbalimbali iliyo mbele yao.
Lucas amesema, mchezo wa kwanza dhidi ya Cameroon utapigwa hapo kesho huku mchezo wa pili ukitarajiwa kupigwa Novemba 13 mwaka huu.
Kikosi cha Twiga Stars ambacho kimewasili jana nchini Cameroon ni
Makipa:
Fatma Omari na Najiat Abbas
Mabeki :
Wema Richard, Sophia Mwasikili, Anastasia Katunzi, Maimuna Hamisi, Fatuma Issa, Happiness Mwaipaja na Mary Masatu
Viungo :
Donisia Minja, Stumai Abdallah, Amina Ally, Anna Mwaisura na Fadila Kigarawa
Washambuliaji:
Fatuma Swalehe, Asha Rashid na Mwanahamisi Omari