
Afisa Habari wa TFF Boniface Wambura
TFF imesema imeafiki maamuzi ya kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) yakuipa ushindi Stand United dhidi ya JKT Kanembwa baada ya timu hiyo kuchezesha wachezaji waliosajiliwa dirisha dogo kwenye mechi yao ya kiporo ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Afisa habari wa TFF Boniface Wambura amesema uamuzi huo ulizingatia sheria na kanuni na JKT Kanembwa walikua wanajua juu ya zuio la kutowatumia wachezaji ambao hawakucheza mchezo wa awali ambao ulivunjika.
