Monday , 28th Jan , 2019

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera ameweka wazi kuwa anahitaji sahihi za wachezaji kadhaa kutoka klabu ya Kariobangi Sharks ili kuimarisha nafasi mbalimbali katika kikosi chake hususani eneo la ulinzi.

Benchi la ufundi la Yanga

Zahera amesema mipango hiyo ya usajili huku akieleza kuwa klabu hiyo imejipanga vyema kuweza kupata fedha nyingi za usajili ili kuboresha kikosi chake.

''Katika klabu ya Kariobangi Sharks nawahitaji wachezaji waliovaa jezi namba 8, 7 na 17 ndio tunatakiwa kusajiliwa'', alisikika Zahera akieleza.

Aidha kocha huyo amesema anataka kusajili wachezaji kwenye nafasi ya mlinzi wa kushoto na kulia pamoja na mlinzi wa kati ili kukipa nguvu kikosi chake.

Yanga ilitolewa katika robo fainali ya michuano ya SportPesa na Kariobangi Sharks kwa kufungwa mabao 3-2.