
Hanspope (KUlia) akimkabidhi Tshabalala zawadi ya gari
Mzozo amesema kwamba Hans Pope amefanya jambo jema ambalo linafaa kupongezwa hasa baada ya kutambua mchango wa mchezaji kwa kuwa jambo hilo litampa faraja kubwa mchezaji mwenyewe na kuendelea kuitumikia vyema timu ya Simba.
Amesema kwamba mbali na kumkabidhi gari, pia amempa shilingi milioni moja fedha za Tanzania kwa ajili ya kumsaidia kununua mafuta ya gari hiyo.