Tuesday , 12th Jul , 2016

Katika kuhakikisha mkoa wa Iringa unapata klabu ya ligi kuu ya soka Tanzania bara mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka viongozi wa klabu hiyo kuweka pembeni tofauti zao na kuungana kwa pamoja ili kuepukana na aibu ya kila mwaka.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela

Kasesela amesema amewaambia wadau wa mpira mkoa wa Iringa kwamba kumekua na changamoto kubwa kwa sasa kutokana na hali halisi ya kiuchumi hali inayopeleka viongozi klabuni hapo kurushiana mpira wa lawama kusaka mchawi wao .

''Ugomvi mnaouona sasa ni kwa kuwa tupo huku chini lakini tukishikamana tukahakikisha timu yetu inakwenda ligi kuu malumbano yatapungua na tutajikita kuhakikisha timu yetu inafanya vizuri''- Amesema Kasesela.

Aidha Kasesela amewataka wadau wa mpira waliomo mkoani Iringa na ambao wapo nje ya mkoa huo kushikamana kwa pamoja ili kuhakikisha timu yao inapanda daraja kwa kuichangia fedha na kutoa mali zao kwa hali na mali.