Tuesday , 31st May , 2016

Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT), limelisimamisha kwa mwaka mmoja Shirikisho la Masumbwi la Ngumi za Kulipwa nchini (PST) kujishughulisha na mchezo huo baada ya kugundulika kukiuka kanuni na sheria za mchezo husika.

Katibu Mkuu wa BMT Mohamed Kiganja.

Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT), limelisimamisha kwa mwaka mmoja Shirikisho la Masumbwi la Ngumi za Kulipwa nchini (PST) kujishughulisha na mchezo huo baada ya kugundulika kukiuka kanuni na sheria za mchezo husika.

Katibu Mkuu wa BMT Mohamed Kiganja amesema uongozi wote wa PST hautaruhusiwa kujishughulisha na masumbwi baada ya kuwachezesha mabondi wenye umri chini ya miaka 18 jambo ambalo ni kinyume na utaratibu.

Aidha, Kiganja amesema Baraza la Michezo la Taifa limetengua ukatibu wa Emmanueli Mlundwa katika kamati ya ngumi za kulipwa maamuzi yaliyoanza kuanzia hii leo.