
Programu ya FaceApp
Agizo la kuchunguzwa kwa programu hiyo limetolewa na Seneta mwandamizi katika Jiji la New York nchini humo, Chuck Schumer, ambapo amekiagiza kitengo cha uchunguzi wa ndani na ulinzi (FBI) kuichunguza programu hiyo kufuatia kile alichokidai ni tishio la kiusalama.
Seneta huyo amedai kwamba programu hiyo inamilikiwa na kampuni ya nchini Urusi, ambako ndiko yaliko makao yake makuu na kudai kuwa kuna uwezekano wa kutokea hatari kwa watumiaji wake, ikiwemo kudukuliwa taarifa zao.