Sunday , 6th Jul , 2014

Wanamuziki maarufu wa muziki wa dansi nchini Tanzania Allan Mulumba Kashama na Totoo Ze Bingwa wameungana kwa pamoja na kuunda kundi jipya walilolibatiza jina 'Bonavida Brothers' ambalo limeanza kuwateka mashabiki na wadau wa muziki Afrika Mashariki.

Wanamuziki Totoo ZeBingwa na Alain Mulumba

Allan Mulumba ameongea na eNewz kuwa kundi hilo ambalo linapiga miondoko ya Afro Pop limetoa kichupa chao kipya ambacho kimefanyiwa kazi na Joe Studio na Ogopa Production kilichobatizwa jina 'My Life'.