Thursday , 19th Feb , 2015

Franklyn Emuobor, raia wa Nigeria aliyetangazwa kukamatwa kwa kosa la kusambaza picha za utupu za msanii wa muziki Desire Luzinda, ameibuka na kukanusha taarifa hizo zilizotolewa na Waziri wa Maadili Uganda Mchungaji Simon Lokodo.

Franklyn na Desire enzi za penzi lao

Katika kuthibitisha hilo, Franklyn ambaye yupo kusipojulikana amerekodi video fupi na kuisambaza akitoa maneno ya kejeli kwa waziri huyo, na kusababisha mkanganyiko huku watu wengine wakitaka waziri huyo awajibike ama kufafanua kinachoendelea.

Franklyn pia ametumia njia ya mtandao kumnanga Desire aliyekuwa mpenzi wake kuwa, picha ya nyumba iliyo katika ujenzi aliyoiweka mtandaoni hivi karibuni sio ya kwake kwakuwa mwanadada huyo hafahamu hata bei ya simenti.