Saturday , 2nd May , 2015

Wakati kukiwa na mabishano makubwa mitaani kuhusu mpambano wa kihistoria wa Ngumi kati ya Manny Pacquiao na Floyd Money Mayweather, limeilazimu Enews kupima joto lake juu ya ni nani anayepatiwa nafasi kubwa ya kushinda katika pambano hilo

Floyd Mayweather na Manny Pacquiao

Majibu ya Cyrill Kamikaze baada ya kuulizwa ni nani anaweza kushinda mpambano huo, ni kuwa kila mmoja anaweza kuchukua ushindi endapo atakuwa makini na kusoma game ya mwenzake, ambapo kwa ufafanuzi zaidi, unaweza kutazama alichokisema kupitia link hii https://www.youtube.com/watch?v=R3F4i74Bol0

Prince Dully Sykes kwa upande wake, ameweka wazi kuwa ni Team Pacquiao, itokee bondia huyo ameshinda ama ameshindwa, huku akiweka wazi kuwa havutiwi na maneno mengi na mbwembwe za Mayweather.

Hayo ni baadhi tu ya maoni ya mastaa wetu, unafikiri ni nani atashinda mpambano huu, tafadhari weka maoni yako hapo chini.