
King Dee ambaye anatamba na nyimbo mbili zilizovuma sana zijulikanazo kwa jina la 'Siko kamili' na ' Nipe Tamu' anaamini kuwa katika wasanii wanaotarajiwa kuwa wakubwa Afrika Mashariki yeye ni miongoni mwao maana anasema ana kipaji kikubwa na anajua kufanya muziki mzuri.
" Napenda watu wafahamu kwamba nimejipanga kufanya muziki mzuri na wataupenda sana, hata kama mtu aliyesikiliza nyimbo zangu za Nipe utamu na siko kamili ataelewa kitu gani namaanisha, nimejipanga kuiletea Afrika Mashariki tuzo nyingi sana za ndani na nje maana ninajiamini ninaweza kufanya hilo kupitia muziki wangu" alisema King Dee
King Dee ameomba watu kutoka nchi za Afrika Mashariki na nje waweze kumpa sapoti kubwa maana anaamini hatowaangusha na anamini sapoti yao ndio itafanya yeye aweze kufika mbali zaidi
Unaweza kubofya hapa kuusikiliza wimbo wake huu wa Nipe tam https://www.youtube.com/watch?v=eAxW_VZRTuM&feature=youtu.be
