Thursday , 18th Sep , 2014

Msanii wa miondoko ya Bongofleva Akil Ze Brain wa nchini Tanzania ambaye amekuwa kimya kwa muda akijiandaa kutoka na kazi mpya tayari amekamilisha kichupa chake kipya alichokibatiza jina 'Habibty' alichomshirikisha msanii maarufu nchini Saraha.

Msanii wa bongofleva nchini Akil Ze Brain

Akili ameongea na eNewz kuwa kichupa hicho kipya kimefanyiwa kazi chini ya muongozaji mahiri Frank Obhthani kutoka Outcome Video Production, huku audio wa wimbo huo ukipikwa katika studio yake Akil iitwayo Akil Records.

Kichupa hicho ambacho kimefanyiwa upigaji picha Visiwani Zanzibar kitazinduliwa rasmi kwa mara ya kwanza kesho Ijumaa usiku katika show yako bomba ya Friday Night Live ya EATV.