Friday , 28th Oct , 2016

Mkuu wa wilaya ya Hanang Sarah Msafiri ametoa saa 24 kwa wavamizi wa shamba la muwekezaji la gidagamouwd katika kijiji cha ming’anyi kuhakikisha wameondoka katika eneo hilo bila kuhatarisha amani kwa wakazi wa kijiji hicho.

Mkuu wa wilaya ya Hanang, Sara Msafiri

 

Imeelezwa kuwa mnamo tarehe 30.4.2013,wavamizi hao wapatao 115,walikubali kuondoka katika eneo hilo lakini mpaka sasa hawajatekeleza makubaliano hayo.

Shamba hilo lenye thamani ya milioni 800, hekari 16,000 limevamiwa na baadhi watu kutoka miji jirani ya wilaya hiyo na kuchukua hekari 450 kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kilimo bila idhini ya muwekezaji huyo.

Aidha kwa upande wa muwekezaji wa shamba hilo Rilash Kalaiya amesema kuwa bado wana uwezo wa kuliendeleza shamba hilo na kuiomba serikali kudumisha usalama wao ili kuweza kuendelea na shuguli za uzalishaji wa mazao kama awali.