
Majeruhi huyo alikuwa akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (Moi) baada ya ajali iliyotokea usiku wa jana Juni 11, 2018.
Ofisa uhusiano wa Moi, Patrick Mvungi amesema waliwapokea majeruhi hao saa 9:30 usiku wakitokea Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), amewataja majeruhi hao kuwa ni Abishai Nkiku (24), mwanafunzi wa UDSM na Jonathan Lugando (40), mhudumu wa chuo hicho.
"Madaktari wanaendelea kumhudumia Nkiku ingawa ameumia sana kichwani,” amesema Mvungi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Daruso waliofariki awali katika ajali hiyo ni Maria Gordian ambaye alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza na Steven Sango wa wa mwaka wa pili.