
Msemaji wa Riek Machar,(Kushoto),Bw. James Gatdet Dak
Katika taarifa yake, UNHCR imesema hofu hiyo inazingatia kuwa Bwana Dak alishapatiwa hadhi ya ukimbizi nchini Kenya na kwamba kitendo cha kulazimishwa kuondoka ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa za ukimbizi.
UNHCR imesema jitihada za kuomba serikali ya Kenya kubadili uamuzi huo hazikuzaa matunda na hivyo walichofanya sasa ni kuisihi serikali ya Sudan Kusini ihakikishe haki za binadamu za Bwana Dak zinazingatiwa.