Monday , 3rd Aug , 2015

Maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana wa kike wenye umri wa kati ya miaka 15 na 39 mkoani mbeya yameongezeka kwa zaidi ya mara tatu ikilinganishwa na vijana wa kiume wenye umri kama huo katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho

Utafiti ambao umefanywa na tume ya taifa ya kudhibiti ukimwi, tacaids, umebaini kuwa kasi ya maambukizi ya ukimwi kwa vijana wa kike mkoani mbeya ni kubwa ikilinganishwa na vijana wa kiume.

Akizungumza na chombo hiki mratibu wa ukimwi mkoani mbeya, stella kategile ameeleza sababu ya kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa mtoto wa kike mkoani mbeya kuwa juu ikilinganishwa na mtoto wa kiume

Kwa mujibu wa takwimu za kitaifa, mkoa wa mbeya unashika nafasi ya tatu kwa kuwa na maambukizi makubwa ya ukimwi nchini, ukitanguliwa na mkoa wa dar es salaam na iringa.