Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga
Bi. Nkinga ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa mashauriano wa kanda ya Afrika kuhusu Mtandao wa Kuzia Unyonyaji na Usafirishaji wa Watoto ambapo amesema Tanzania inapata sifa hiyo kutokana na kuridhia kutekeleza mikataba mbalimbali ikiwemo kutunga sera na sheria pamoja na mikakati ya kupambana na ukatili dhidi ya watoto.
Aidha amezitaka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wa kufanya tafiti za ukatili dhidi ya wanawake na watoto barani Afrika ambapo amezitaja nchi nyingine zinazotajwa kuwa mfano wa kuigwa kuwa ni pamoja na Mexico, Indonesia na Sweden.